Overblog
Edit post Follow this blog Administration + Create my blog
liturjia-takatifu.over-blog.com's name

Hii blog ni kwa ajili ya kuitikia mwaliko wa Mtaguso wa pili wa Vatikano wa kuwafanya wakatoliki wote waifahamu liturjia takatifu wanayoiadhimisha. Nitatoa utafiti wangu juu ya liturjia na nitakuwa tayari kujibu maswali yenu juu ya liturjia. Karibuni sana!The aim of this blog is to impart liturgical knowledge to the people of God. It targets mainly the people from the swahili speaking countries. Welcome for the sharing of knowledge about our liturgy!

Machweo ya jua huko Kifuru Dar es Salaam: Mtazamo wa Muda na Mazingira yetu

  Mungu ametubariki sana watanzania na waafrika kwa ujumla. Unaona jinsi jua linavyotoka kwa muda muafaka na kuzama kwa muda muafaka. Summer hii nipo Ujerumani kwenye mji ujilikanao kama Wolfenbüttel. Watu ni wema na wanapenda sana watanzania na nchi yetu ya 27062008101-copy-1.jpgTanzania. Kila mwaka tunakuwa na Misa ijulikanayo kama "Afrikanische Messe". Kwenye hii Misa tunaimba nyimbo za Kiswahili na lugha nyingine za Kiafrika. Mwisho wa Misa watu ukaa pamoja na kuwa na mlo wa pamoja wa mchana. Tunawaeleza sana mambo ya kwetu nao wanafurahi sanas.


Lakini huku sasa hivi jua linazama saa 4 na kitu usiku. Yaani kwangu inakuwa shida sana kusinzia. Kwani najisikia kama kulala saa 12  na nusu jioni nikiwa nyumbani (Tanzania), lakini saa inaonyesha saa 5 usiku. Maajabu hayo. Tena nasikia kaskazini zaidi huko basi kwa sasa ni mchana tu masaa yote. Nimeshuhudia hilo nikuwa kwenye ndege nikisafiri kutoka Nice (Ufaransa) kwenda Hannover (Ujerumani) saa 6 usiku, niliona mwanga wa jua huko maeneo ya Kaskazini mwa dunia yetu. Nadhani ingekuwa Tanzania watoto wangecheza mpira wa miguu usiku kucha na wazazi wasingelalamika kwa sababu hakuna giza. Basi wangeenda shule wakiwa wamechoka. Ng'ombe, mbuzi, Kuku  na wanyama wengine wangekula masaa 24.  Kwa wale waliosoma Rubya Seminari miaka ya nyuma,  basi tungepiga "msipaka" (Kupiga msipaka ni kusoma usiku wakati wengine wamelala) bila gharama ya mafuta ya taa. Lakini je, asubuhi mtu angeamkaje? Wavuvi wa dagaa wangepata hali ngumu kama mwezi tu unawasumbua. Kwenye meli ya Victoria au Serengeti, daraja la kwanza na la pili kulala wangekosa wateja kabisa. Tukumbuke kuwa wakati wa majira ya baridi huko ni giza masaa mengi au hata yote! Sijui hali yetu ingekuwaje! Basi tufurahie mazingira yetu na tuyaboreshe ili tuishi kwa furaha na hali bora zaidi. Mungu ametupa uwezo wa kuboresha mazingira yetu, sema tu mara nyingine hatutumii kabisa uwezo huo.

 

Kutokana na hali hiyo ninayoipata sasa nitaandika juu ya mtazamo tofauti wa muda wa watu mbalimbali duniani. Tofauti hii inatokana na tofauti ya mazingira, utamaduni na shughuli za kila siku. Mkulima atakuwa na mtazamo tofauti wa muda na mvuvi au mwindaji. Mkulima shughuli zake ni mchana na mvuvi mara nyingi ni usiku (Nazungumzia hasa wavuvi wa mkoa wa Kagera katika ziwa Victoria nilio na uzoefu nao).


Naomba mchango wa mawazo yenu juu ya muda (Time Concept) ili niweze kufanikisha mpango huo nilio nao. Nitaanza na mada ifuatayo kwa Kiingereza "Liturgical Year and Bahaya Concept of Time". Kichwa hiki sijakiweka vizuri lakini ndiyo nia yangu ya kuandika juu ya Muda katika mila za Wahaya wa kale na wa sasa. Nitajaribu kuoanisha na mtazamo wa Mwaka wa Kanisa (Latin Rite). Ninajaribu kutafiti ni jinsi gani tunaweza kuoanisha Ukristu wetu na Utamaduni wetu ulio mzuri hasa katika mzunguko mzima wa mwaka.


Tunaweza kujiuliza swali, Kwa nini kila mwaka hasa Desemba karibu na Krismasi au Noeli, huwa inakuwa vigumu kupata tiketi ya kusafiri kwenda mikoani? Je, watu wanaosafiri kipindi hicho wanaenda tu kusherekea Krismasi nyumbani au kuna mambo mengine ambayo yameunganishwa kwa nia nzuri na siku hiyo? Kama huamini jaribu kwenda Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo mwisho wa mwaka, ulizia tiketi ya Bukoba, Mwanza, Moshi au Arusha na utanipa jibu. Nadhani kwa mtazamo wangu, ambao bado naufanyia utafiti zaidi, kuna jambo zuri tu la kimila ambalo limeunganishwa na sherehe ya Krismasi na mwisho wa Mwaka.


Nami kwa upande wangu natamani sana kufanya sana utafiki juu ya mtazamo wetu wa muda kwa ujumla na kuhusu mambo ya imani yetu. Karibuni katika mjadala huu kwa kutoa mawazo, habari muhimu, taarifa, hadithi na maswali juu ya mada hii.


G. Mutarubukwa
27062008101
by ijue-liturjia-takatifu.over-blog.com

Share this post
Repost0
To be informed of the latest articles, subscribe:
Comment on this post
A
<br /> Mh. Padre nakushukuru kwa jitihada zako kama hizi kuweka katika mtandao makala kuhusu liturjia. Nimesoma kwa haraka sana na nimeona yapo makosa ya kuandika mfano ... katika chuo kama kila<br /> (natumaini ni KILE). Nitaendelea kutembelea blog yako. Nakutakia utume mwema.<br /> <br /> <br />
Reply
I
<br /> <br /> Nashukuru sana Mh. Padre Athanasius; nitafanya marekebisho ya makosa hayo sasa hivi. Nakutakia usomaji mwema na karibu kwa mchango wa mawazo. Nakutakia utume mwema na likizo njema.<br /> <br /> <br /> Fr. Gerald<br /> <br /> <br /> <br />
J
<br /> Dear Fr Gerald, It is a great pleasure to hear from you especially with this blog on Liturgy as we had proposed during our days at Sant'Anselmo in Rome while studying Liturgy. We Africans must do<br /> something so that we can uplift our concepts on Liturgy and most especially to get a chance to express ourselves. We are very lucky with our concempt of time because it is so near to that of Christ<br /> our saviour(during His time). So we must use this chance to the maximum to inculturate the Liturgy.<br /> <br /> God bless!<br /> John Bosco Katabaazi Mpungu<br /> <br /> <br />
Reply
I
<br /> <br /> Hallo Fr. John Bosco,<br /> <br /> <br /> Thanks very much for your comment. It was very nice to hear from you. Yes it is high time that we do something to make sure that our Christianity becomes strong through liturgy by working hard on<br /> liturgical inculturation. The blog we began at Sant'Anselmo was not successful as people did not contribute to its development. I hope you are fine and doing well.<br /> <br /> <br /> All the best and God bless!<br /> <br /> <br /> Gerald Mutarubukwa<br /> <br /> <br /> <br />
K
<br /> Nimefurahia sana jinsi unavyooanisha liturjia na maisha ya kawaida ya kila siku. Watu wengi watanufaika na hii blog ya ijue liturjia, mimi nitakuwa mteja namba moja. Bravo Bro.<br /> <br /> <br />
Reply
G
<br /> Inabidi kweli sis waafrika au Watanzania kumshukuru sana Mungu maana majira yote ya mwaka tunaweza kuendelea na shughuli zetu kama kawaida.<br /> Hapa Harbin, China winter ndiyo ndefu kuliko majira mengine, kwa hiyo wanaofanya shughuli zao nje (yaani kama vile machinga) wanafunga biashara zao mpaka spring ianze. Kwahiyo sisi tuna muda mwing<br /> inabidi tuangalie jinsi ya kwenda na wakati.<br /> Naomba nichangie namna hii.<br /> <br /> <br />
Reply
E
<br /> Blog hii itakuwa na manufaa sana kwa waamini wetu. Tunasubiri kwa hamu kubwa.<br /> <br /> <br />
Reply